Hesabu zawakimbiza wanaosoma Ugavi - VAN NEWS

Latest

Sunday, 7 January 2018

Hesabu zawakimbiza wanaosoma Ugavi

BODI ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imesema udahili wa wanafunzi wanaofanya mitihani ya bodi hiyo umepungua kutokana na woga wa wanafunzi na somo la hesabu kuwa tatizo kubwa kwao.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Bodi hiyo, Godfrey Mbanyi alisema lengo la bodi hiyo ni kudahili wanafunzi waliochukua kozi ya ununuzi na ugavi 2,000, Hata hivyo, alisema tangu mwaka 2016, udahili umekuwa ukishuka ambapo katika mtihani uliofanyika mwaka 2016, walifanya udahili kwa wanafunzi 1,519, waliofanya mtihani ni 1,442, waliofaulu ni wanafunzi 660 na kati yao 745 wanarudia mitihani wakati wanafunzi 37 sawa na asilimia 2.6 walifeli.

No comments:

Post a Comment